JESHI LA POLISI LAMCHUKULIA HATUA ASKARI ALIYECHUKUA RUSHWA KUTOKA KWA RAIA WA KIGENI


Jeshi la Polisi Zanzibar limemkamata askari wake anayetuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa raia wa kigeni baada ya kumkamata kwa kosa la barabarani na kumuachia huku akimuahidi kumlinda.

Uamuzi huo wa jeshi la polisi Zanzibar umetolewa na kamishna mkuu wa jeshi hilo hapa Zanziabr CP Hamdan Omar Makame wakati akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya polisi ambapo amesema jeshi la polisi limesikitishwa sana na kulani kitendo hicho cha askari huyo akipokea rushwa kwa kosa la raia huyo kutovaa mkanda na kitendo hicho kusambazwa kwenye mitandao ambapo amemtaja askari huyo ni sajeti Talib Hamad na siyo jina la Ali huku pia akisema kitendo hicho kilifanyika Mkokotoni na sio Mahonda kama alivyokaririwa askari huyo kwenye mahojiano ya mtandao.

Kamishna mkuu huyo wa polisi Zanzibar amesema kwa sasa askari huyo hatachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu za kipolisi na ikithibitika kuwepo kosa la jinai atapelekwa kwenye vyombo vya sheria vya dola huku na akisisitiza wananchi waendelea kutoa ushirikiano.

Kwa mujibu wa tukio hilo lilivyoonekana kwenye mtandao huo raia huyo alikamtwa kwa kosa la kutovaa mkanda wa gari na askari huyo aliamua kuchukua leseni ya barabara na kumuhakikishia kuwa aendele na safari na atamlinda huku akionekana akipokea fedha taslimu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment