KABILA KUTUA TZ LEO,APANGA KUYAONA MABADILIKO YA BANDARI YA DAR ES SALAAM..!!!


RAIS Joseph Kabila, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), anatarajia kuwasili nchini leo kwa ziara ya siku tatu.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, alisema Rais Kabila atapokelewa na Rais John Magufuli kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Makonda aliwaambia wanahabari jana kuwa katika ziara hiyo, Kabila atazungumza mambo mbalimbali na mwenyeji wake na kesho atatembelea Bandari ya Dar es Salaam.

Licha ya Rais Kabila, Makonda pia alisema Makamu wa Rais wa Cuba, Salvador Mesa ataingia nchini kwa ziara ya siku mbili na atapokelewa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Pia alisema katika mkoa huo kuna ugeni wa waumini wa Mabohora zaidi ya 30,000 ambao wanafanya Mkutano Mkuu nchini baada ya kukubali ombi la Rais Magufuli la kufanyia mkutano wao nchini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment