Wakati
Kampeni za kinyang’anyiro cha kuingia Ikulu ya White House zikiendelea
kupamba moto nchini Marekani huku kila mgombea akijinadi kwa Wamarekani
kwa kumkosoa mpinzani wake.
Donald
Trump amevishutumu vyombo vya habari nchini humo kwa madai kuwa
vimeripoti habari za uwongo dhidi yake kwamba aliwadhalilisha wanawake
kingono. Tuhuma hizo dhidi ya Trump zilitolewa wakati mke wa rais Barack
Obama, Michelle Obama akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni ya
kumpigia debe mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton mjini New
Hampshire.
Katika
mkutano huo Michelle Obama alimshambulia kwa ujumbe mkali mgombea huyo
wa Republican kwa kudai kuwa, Trump anastahili kukomeshwa tabia yake ya
kudhalilisha wanawake huku akisisitiza kuwa hajatoa shutuma hizo kwa
sababu Trump yupo chama pinzani.
“Haijalishi
uko chama gani, Democratic, Republican, au asiye na chama. Hakuna
mwanamke anayestahili kufanyiwa hivi, aina hii ya dhuluma. Nafahamu hii
ni kampeni, lakini hili halihusu siasa, ni kuhusu maadili ya ubinaadamu,
ni kuhusu kizuri na kibaya na hatuwezi kuendelea kuvumilia hilo au
kuwaweka watoto wetu katika hali hii sio tu dakika moja bali miaka minne
ijayo. Ni wakati wa sisi sote kusimama na kusema inatosha sasa”.
alisema Bi Obama.
Lakini
Trump mwenye umri wa miaka 70 alisimama kidete, akiwakemea wakosoaji
wake kuwa ni “waongo wakubwa” na kumshtumu Bi Clinton kwa kula njama na
vyombo vya habari ili kuhujumu kampeni yake.
Hata
hivyo, karibu wanawake sita wametuhumu Trump kwa kujaribu kuwapapasa na
kuwabusu kwa lazima katika matukio yaliyoripotiwa na vyombo vya habari
vya New York Times, NBC, People Magazine.


0 comments :
Post a Comment