Mabingwa
watetezi wa VPL, Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara, Yanga, leo Oktoba 26
imeendeleza wimbi la kutoa dozi kwa timu inayokutana nayo ambapo
wameitandika bila huruma timu ya Maafande Ruvu JKT bao 4-0, mchezo
uliomalizika jioni hii.
Mchezo
huo wa kiporo uliochezwa katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam,
Wanajangwani hao wameweza kushuka kwa mara ya kwanza bila ya Kocha wao
Mholanzi Hans van de Pluijm ambae amejiuzulu baada ya Klabu hiyo
kumwingiza ‘kinyemela’ Kocha Mpya kuchukua nafasi yake.
VPL hivi sasa inaongozwa na Simba wenye Pointi 29 kwa Mechi 11 na Yanga wapo Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 21 kwa Mechi 10.
Awali
Yanga, waliibamiza Kagera Sugar 6-2 katika Mechi yao iliyopita, hivyo
kwa ushindi wa leo wa bao 4 ni kielelezo tosha cha kuendeleza dozi.
Wapinzani wao wa jadi Wekundu wa Msimbazi wao wanashuka Jumamosi ya Oktoba 29 wakicheza Ugenini huko Shinyanga na Mwadui FC.
Kipigo
hicho cha bao 4, kinaendelea kuiweka Ruvu JKT kizani kwani hadi sasa
imeshinda Mechi 1 tu, Sare 6 na Kufungwa 5 hali iliyowaacha Nafasi ya
Pili toka Mkiani hadi sasa.


0 comments :
Post a Comment