Ijue Adhabu waliompa Man United shabiki wao kwa kujaribu kuuza tiketi online

Moja kati ya headlines zilizoingia katika soka ni kuhusiana na klabu ya Man United kutangaza adhabu kwa shabiki wake ambaye alijaribu kuuza tiketi ya mchezo wa Man United dhidi ya Fenerbahce online, shabiki wa Man United alijaribu kuuza tiketi yake ya mchezo wa ugenini.
Kama utakuwa unakumbuka mwanzoni mwa msimi Man United walitangaza kuwa kuuza tiketi ambayo tayari ulishauziwa kwa mtu mwingine ni kosa na ikitokea shabiki akafanya kosa hilo atafungiwa kuhudhuria mechi za Man United za nyumbani na ugenini kwa miaka mitatu.
screen-shot-2016-11-18-at-1-23-05-pm
“Kufuatia mchezo wetu wa ugenini dhidi ya Fenerbahce tiketi iliyokuwa imesajiliwa kwa jina lako kutangaza kuiuza kupitia mitandao ya kijamii ni kosa, kwa mujibu wa masharti utafungiwa miaka mitatu kuhudhuria mechi zetu na kufutiwa tiketi yako ya msimu pasipo kulipwa fidia”
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment