VIDEO: Wenger kashindwa kuvunja rekodi yake mbovu dhidi ya Jose Mourinho




Ligi Kuu England imeendelea tena leo November 19 2016 baada ya mapumziko ya muda mfupi ya kupisha mechi za kimataifa zilizopo katika kalenda ya FIFA, mchezo wa kwanza wa EPL kuchezwa weekend hii ulikuwa ni mchezo kati ya Man United dhidi ya Arsenal.
2913
Mchezo wa Man United dhidi ya Arsenal umechezwa katika dimba la Old Trafford, huo ulikuwa ni mchezo ambao unatazamiwa rekodi ivunjwe au iendelezwa kati ya Mourinho dhidi ya Wenger, kama utakuwa unakumbuka vizuri Arsene Wenger hajawahi kumfunga Jose Mourinho katika EPL.
3500
Licha ya wengi kutarajia historia tofauti mchezo umemalizika kwa sare ya goli 1-1, goli la Man United likifungwa na Juan Mata dakika ya 68 , wakati goli la Arsenal lilifungwa na Oliver Giroud dakika ya 88.
screen-shot-2016-11-19-at-5-35-26-pm
Msimamo wa EPL baada ya matokeo ya mechi ya Man United vs Arsenal
Kwa sasa Jose Mourinho anakuwa kacheza jumla ya mechi 16 dhidi ya Arsene Wenger na kufanikiwa kumfunga mechi 8, sare 7 na amekubali kufungwa katika mchezo mmoja tu wa Ngao ya Hisani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment