Staa wa Genk atakayejiunga na Leicester January 1, mashabiki wameanza kumuaga


Taarifa ambayo imeenea katika mitandao ya kijamii na baadhi ya mitandao ya habari za michezo ya England ni kuhusiana na kiungo wa kimataifa wa Nigeria anayeichezea KRC Genk ya Ubelgiji Wilfred Ndindi kuripotiwa kukaribia kujiunga na Leicester City January 1 2017.
wildred-ndidi-leicester-city-transfer-done-deal-747618
Stori kutoka express.co.uk inaripotiwa kuwa Ndindi tayari amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Leicester City kinachosubiriwa ni kutangazwa rasmi January 1 2017, Ndindi anajiunga na Leicester City kwa dau la pound milioni 15, Ndindi amecheza jumla ya mechi 33 akiwa na Genk na kufunga goli 3, Ndindi atakuwa mbadala wa Ng’olo Kante aliyejiunga na Chelsea.
wilfred-ndidi-leicester-city-transfer-done-deal-769329
Mtu wa karibu na Ndindi amenukuliwa na express.co.uk kuwa Ndindi kacheza mchezo wa mwisho akiwa na Genk dhidi ya KAA Gent na atasafiri January 1 kwenda kufanya vipimo, habari ambazo zinapata uzito kutokana na baadhi ya mashabiki wa Genk instagram wameanza kumuaga, Ndindi pia alikuwa anahitajika na Man United.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment