NA  BASHIR  YAKUB -
Sheria   inaruhusu  kutumia 
ardhi  ya  mtu 
kukopea.  Kwa  maana  mtu 
ataomba  hati  yako   au 
nyaraka   yako   yoyote 
ile  ya  umiliki 
halafu  ataitumia  kukopea. Inaitwa Rehani  ya  mtu  wa 
tatu( third party mortgage).   Kifungu 
cha  113 ( 2 ) cha  Sheria 
ya  Ardhi  Na, 4 ya 1999 
kimeeleza kitu  hiki. Hata  hivyo 
yapo  mambo  tunayotakiwa 
kujua  katika  mchakato 
huu  wote. 
Ili  mambo  yaende 
vizuri  kutatakiwa kuwapo  mikataba 
ya  aina  tatu 
kama  tutakavyoona  hapa 
chini.
1.MKATABA  WA  MKOPO.       
Mkataba  wa  mkopo 
( Loan  agreement)  ni 
mkataba   kati  ya   mwomba 
mkopo  na   na 
taasisi  ya  fedha 
inayotakiwa  kutoa  mkopo.  
Mkataba  huu  utakuwa 
na  masharti   ya  
mkopo  kuhusu  urejeshaji, muda  wa 
kurejesha, viwango  vya  riba, 
adhabu  za  kupitisha 
muda  wa  rejesho, muda 
ambao  mkopo  utadumu,  nini 
kitafanyika  iwapo  mkopaji 
atashindwa  kurejesha, haki  na 
wajibu  wa  mkopaji 
pamoja  na  mkopwaji.
Ifahamike kuwa 
masharti  ya  mkopo   
hayafanani.  Yanatofautiana  kutoka 
taasisi  hadi  taasisi   na  pia yanatofautishwa  na 
kiwango   cha  mkopo 
pamoja  na  mazingira 
yote  yanayouzunguka huo  mchakato. Huu 
ni  mkataba  wa 
kwanza.
2.   MKATABA 
WA   REHANI.
Huu  ni  mkataba 
wa  pili. Mkataba  wa 
rehani ( mortgage deed ) utakuwa  ni 
kati  ya  taasisi 
ya  fedha  na 
mtu  anayeweka  rehani. Kwahiyo  kama 
wewe  unamdhamini  mtu 
kwa  kumpa  nyumba 
au  shamba  lako 
ili  akakopee   basi 
unatakiwa  kusaini  mkataba 
huu.  
Yule  ambaye  jina lake 
linaonekana  kwenye  nyaraka  ya 
umiliki  ndiye  anayetakiwa 
kusaini   mkataba  huu.   
3.   MKATABA  KATI 
YA   ANAYEDHAMINI  NA 
ANAYEDHAMINIWA.     
Aidha  usimkabidhi  mtu 
hati  yako  akakopee 
bila  kuwa  na 
makubaliano  ya  kisheria na 
huyo  mtu.  Ni 
hatari  sana  kufanya 
hivi   na   unaweza 
kupoteza  na  wengi 
wamekwishapoteza.  
Wengi  wanachojali  ni 
mtu  achukue  hela  benki  na 
wewe  akupe  asilimia 
zako  mlizokubaliana  basi 
muishie  hapo.  Ukifanya 
hivi  utakuwa  umekosea 
sana.
Wengine  huaminiana  tu  kwa
 urafiki 
au  undugu  na kufanya 
mchakato  huu  bila 
makubaliano  maalum.  Hii 
si  sawa  na 
ina  madhara  makubwa.
Hakikisha unamsainisha 
mkataba  huu na  hakikisha 
mkataba unakuwa  na  vipengele muhimu na  vya 
kisheria  vya  kukulinda 
wewe na  mali  yako. 
Moja  ya  kipengele 
muhimu  ni kueleza  wazi 
ikiwa  atashindwa  kulipa 
deni  huko  alikokopa 
ni  kitu  gani  
kitakulinda  ili  mali 
yako  isiuzwe   au 
hata  ikiuzwa  wewe 
utapata  nini  kutoka 
kwake  kufidia  hiyo  hasara.
4.   MADHARA.       
Madhara  makubwa  unayoweza 
kupata  ni  pale  
atakaposhindwa  kulipa  mkopo. 
Hapa  bila  huruma nyumba/shamba  lako 
litauzwa   na hautakuwa 
na  chochote  cha 
kukulinda  kama  mdhamini. 
Wengi  imewatokea hii  na 
aidha  wamekubali  mali 
zao  ziuzwe  au 
wamelazimika  kumlipia  mtu  deni  ili 
kuokoa  mali  zao.
Pia  mara  nyingi 
watu  wanaokopea  mali 
za  watu   wana 
tabia  ya kukimbia/kupotea au  kuwa 
wajeuri  pale   wanaposhindwa   au 
kuyumba  katika  marejesho. 
Na wanakimbia  wakiwa  huru 
kabisa   wakijua   kinachofuata 
ni  kuuza  mali 
ambayo  kimsingi  anajua sio 
ya  kwake  na 
hivyo  hana  la kupoteza. 
Wewe  usiingie  katika 
majaribu  haya  weka mpangilio  mzuri  wa 
kisheria  ikiwa  utaamua 
kumdhamini  mtu.
5.     UWEZO  WA 
KUZUIA   MALI  YAKO 
ISIUZWE.            
Ikiwa  ulimdhamini  mtu  na
ameshindwa  kulipa  na 
sasa   wakopeshaji  wanataka kuuza  mali  
unaweza  kwenda  mahakamani 
kuzuia uuzaji.   Lakini  utawezaje  na 
hali  uliusaini   mkataba 
wa  rehani( mortgage  deed). 
Niseme  tu  utaweza 
iwapo  tu  una 
sababu  za  msingi  
na  za  kisheria 
na  sehemu  ya 
kusimamia( Locus  stand). 
Aidha  suala  la 
msingi  kuliko  yote 
ni kujihadhari  sana  na 
mpango  huu  wa 
kudhamini  kwa   kutumia 
mali  yako  kukopea. Yawezekana  nawe 
unataraji  kutengeneza  faida 
kupitia  hilo,  ni 
jambo  zuri  ila 
hakikisha  unaweka  misingi 
mizuri  ya  kukulinda wewe na  mali 
yako. 


0 comments :
Post a Comment