Everton Kutua bongo kesho asubuhi



Timu ya Everton itatua nchini kesho asubuhi tayari kukabili Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa kirafiki wa Sportpesa utakaofanyika kwenye Uwanja wa  Taifa jijini Dar es Salaam.


Baada ya kuwasili timu hiyo  mchana  itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa  Taifa, lakini  hautaruhusu mtu yoyote kutazama mazoezi yao.

Afisa usalama viwanjani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)  na Shirikisho la Soka Duniani (Fifa), Hashim Abdallah aliwataka mashabiki wa soka kutii agizo la timu hiyo kwa kutulia nyumbani na kusubiri siku ya mchezo.

"Everton wameshatoa maelekezo kuwa  mazoezi yao hawataruhusu mtu yoyote kuangalia hivyo  mashabiki wa soka wanapaswa kutii hilo ili wasiingie katika vita na jeshi la Polisi.

"Pia mashabiki wanatakiwa kununua tiketi mapema ambazo zimeanza kuuzwa leo kupitia Selcom ili kuepuesha msongamano na  vurugu siku ya mchezo maana mashabiki wengi wanapenda kununua tiketi siku ya mwisho wakati walikuwa wana muda wa kununu mapema"alisema Hashim.

Hashim alisema wamejiandaa kuimarisha usalama tangu kuwasili kwa timu hiyo mpaka siku ya mechi na  watahakikisha siku hiyo barabara za Kilwa na Mandela  zinapitika kirahisi ili kuwafanya mashabiki kuwahi uwanjani na kuondokana na foleni.

Naye  Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo, Yusuph Singo alisema Serikali  wamehakiksiha uwanja unakuwa katika hali nzuri kwa ajili ya mchezo huo huku mgeni rasmi  katika mchezo huo akiwa ni Makamu wa  Rais, Samia Suluhu.

Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa kampuni ya Sportpesa, Abbas Tarimba  alisema leo mchezaji wa zamani wa Everton , Leon Osman ataendesha semina ya uongozi kwa viongozi wa klabu nchini na itafanyika   Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Julai 12."
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment