Askofu wa Jimbo Katoliki la Zanzibar, Mhashamu Agustino Shao amewataka Watanzania kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa hatua anazochukua kurekebisha mambo muhimu kwa maendeleo ya taifa, licha ya kuwepo kwa changamoto katika kipindi cha mpito.
Baba Askofu Shao amesema hayo leo Jumapili, Oktoba, 15 wakati akihubiri katika Misa Takatifu iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, Parokia ya Minaramiwili ambapo rais Magufuli ameungana na waumini wa Kanisa hilo kusali Ibada ya Jumapili ya Dominika ya 28 ya mwaka A wa Kanisa.
Akitoa mfano wa nchi ya Zimbabwe ambayo Rais wake, Robert Mugabe aliamua kuchukua hatua za kupigania maslahi ya Wazimbabwe na sasa wananchi wa nchi hiyo wameanza kuzalisha bidhaa na kuziuza nje ya nchi, askofu Shao amesema hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli kupambana na rushwa, kupigania rasilimali za Watanzania, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji, kukabiliana na wizi na ubadhilifu wa mali za umma na kubana matumizi, zinapaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.
“Hatutaweza kusema tunaimaliza rushwa wakati tunaendelea kuishi kwa kupata fedha ambazo hujazifanyia kazi, ni lazima tuishi machungu ya kuimaliza rushwa, ni lazima tuishi machungu ya kuweka uadilifu katika utendaji wetu, tusipoishi machungu hayo tutaishi dunia mbili, dunia ya rushwa na dunia ya kujenga uchumi na uadilifu wa Watanzania, tukubali kujikatalia ili tuweze kupata mazuri tuliyotaka” amesema Baba Askofu Shao.
Katika salamu zake baada ya kumalizika kwa Misa Takatifu, Rais Magufuli amemshukuru Baba Askofu Shao kwa mahubiri yake na ameungana nae kuwahakikishia Watanzania kuwa Serikali inachukua hatua za kupambana na rushwa na kulinda rasilimali za nchi ili ziweze kuwanufaisha wananchi wenyewe.
Rais Magufuli amesema hata Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambaye jana ametimiza miaka 18 tangu afariki dunia, alipiga vita rushwa na alipigania rasilimali za nchi, hivyo ametaka Watanzania wote kuungana katika juhudi hizo.
Dkt. Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewashukuru Watanzania wote kwa maombi yao na kuchangia shilingi milioni moja kwa ajili kwaya ya kanisa hilo na shilingi Milioni 5 kwa ajili ya maendeleo ya



0 comments :
Post a Comment