Simba Imemfukuza Kocha wake Omog

 

Simba imevunja mkataba na Kocha Joseph Omog na sasa anaondoka zake kurejea kwao Cameroon.


Simba Sports Club
Dar es salaam
23/12/2017


      TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*
_____________________________________


Klabu ya Simba na kocha wake mkuu Joseph Omog, wameamua kwa pamoja kuvunja mkataba baina yao kwa makubaliano maalum yanayozingatia maslahi ya pande zote mbili. 

Klabu inamshukuru kocha Omog na inamtakia kila la kheri kwenye maisha yake nje ya Simba.

Kwa wakati huu Timu yetu itakuwa chini ya kocha msaidizi Masoud Djuma na itaendelea na mazoezi kesho,na kupumzika siku ya Jumatatu kwa mapumziko ya sikukuu ya Christmas na itaingia kambini Jumanne kabla ya safari ya Mtwara,ambapo tutacheza na Timu ya Ndanda kwenye mchezo wa Ligi kuu wiki ijayo.

Pia kwa niaba ya uongozi, benchi la ufundi na wachezaji.tutumie nafasi hii kuwaomba radhi sana Wanachama na washabiki wetu kwa matokeo ya jana, sote tumeumia ila ndio mchezo wa mpira ulivyo, na tuwaombe muwe watulivu katika kipindi hiki ili tufikie malengo yetu. 

Mwisho

klabu inawatakia nyote Sikukuu njema ya Noeli na mapumziko mema ya wikiendi. 

IMETOLEWA NA.... 

Haji S MANARA
Mkuu wa Habari Simba Sc

SIMBA NGUVU MOJA
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment