Wakongo Wakimbilia Zambia Kutafuta Hifadhi


Zaidi ya watu 12,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamekimbilia nchi jirani ya Zambia kutafuta hifadhi kutokana na machafuko Kusini Mashariki mwa nchi yao.

Umoja wa Mataifa unaonya kuwa, hali ya wakimbizi hao ni mbaya, na wanakosa mahitaji muhimu kwa sababu ya uhaba wa fedha lakini pia kuondelea kuongezeka kwa wakimbizi hao ambapo UNHCR inasema inahitaji Dola za Marekani Milioni 236 Kuwasaidia wakimbizi hao.

Tangu mwezi Agosti pekee, zaidi ya wakimbi 8,000 wameingia nchini Zambia wengi wao wakiwa wanawake na watoto.

Mdororo wa usalama nchini DRC umesababisha raia wengi kuyahama makazi yao ambapo hayo yanajiri wakati ambapo chama kikuu cha upinzani nchini DRC, UDPS kikidai kwamba hakimtambui Waziri Mkuu Bruno Tshibala kama mwanachama na kiongozi ndani ya chama hicho.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment