Mbunge wa Arusha Mjini kupitia CHADEMA Mh Godbless Lema amesema kuna mbunge wa CHADEMA yupo njiani ndani ya wiki hii kukikacha chama hicho na kujiunga na CCM.
Lema ameyasema hayo kupitia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wake wa Twitter uliosema
"Kati ya Jumatano wiki hii na ijumaa,pesaitakuwa na thamani kwa maisha ya mvulana mmoja ambae ni Mbunge kutoka CDM (HADEMA).Mtakaposikia mambo haya msiogope,kwani imeandikwa ktkwatanzani 1:2 inawapasa wote wasio na utu/ hakikuondoka ili ukombozi ule wa kuiondoa CCMutimilike kwenu". Ameandika Lema.
Lakini katika pitapita yangu mitandaoni nimekuta watu wengi wakimhusisha John Mnyika,Mbunge wa Kibambana na sakata hilo kutokana na wiki hii kutajwa mara kwa mara kwenye sakata kama hilo.
0 comments :
Post a Comment