Mahakama Yatoa Maagizo Takukuru Kesi Ya Jamal Malinzi

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) amewarejeshea TAKUKURU jalada la kesi ya utakatishaji wa fedha inayomkabili aliyekuwa rais wa (TFF), Jamal Malinzi na wenzake ili warekebishe vitu vichache vya kiuchunguzi.
Mbali ya Malinzi, wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Msiande Mwanga.
Hayo yameelezwa na Wakili wa TAKUKURU, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, wakati shauri hilo lilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa.
Swai amedai jalada la kesi hiyo limesharudi TAKUKURU likitokea kwa DPP, hivyo wamepewa maelekezo ya kukamilisha baadhi ya uchunguzi.
Baada kueleza hayo, wakili wa Utetezi Nehemia Nkonko aliomba upelelezi wa shauri hilo ukamilike kwa haraka kwa sababu washtakiwa wapo ndani.
Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment