Wednesday, June 24, 2015 Kinana: Wanaoona Misingi ya CCM haifai Waondoke


  Nkupamah blog

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana ameendelea kusisitiza kuwa chama kinarudishwa kwenye misingi yake akitaka mtu anayefikiri misingi hiyo haifai, aondoke atafute mahala pengine.
 
Kinana ambaye katika ziara zake tangu akiwa Kagera, Geita na sasa Mwanza, amekuwa akisisitiza viongozi wa CCM kuhudumia wananchi na kuwatendea haki, alisema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara mjini Sengerema.
 
“Nataka niwahakikishe watanzania tunakirudisha hiki chama kwenye misingi. Na kama kuna mtu anafikiri misingi hiyo haifai, bora aondoke kwenye CCM atafute mahala pengine pa kwenda,” alisema.
 
Akishangiliwa na umati wa watu uliohudhuria mkutano huo, Kinana aliwataka wanasiasa kushikamana kusemea wanyonge. Alisema watu wengi hawana vyama vya siasa isipokuwa wanalazimika kuingia kutafuta maisha.
 
Katibu Mkuu alisema wanachotaka ni kuhakikisha chama kinakuwa karibu na watu, kinawasikiliza na kuwasemea.
 
“Hiki ndicho chama tunachokijua sisi wengine,” alisema na kusihi wana CCM kushikamana katika kusimamia misingi ya watu kwa kupinga mambo ya hovyo na kuunga mkono mambo mazuri.
 
Alisema mtu anayekiri upungufu wake si mtu dhaifu bali ni imara. Alisema si kila jambo linapawa kukubaliwa.
 
“Watu wananyimwa haki yao, sawa, wanadhulumiwa, tuko mbioni,...nataka niwahakikishie watanzania, tunakirudisha hiki chama kwenye misingi,” alisisitiza.
 
Alisema kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira, watu wapate mahitaji yao. Pia alisema serikali inapaswa kusimamia sheria
Nkupamah blog
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment