Barack Obama ziarani Ethiopia

  • Written @nkupamah blog
Alipowasili Ethiopia, Julai 26, 2015, rais wa Marekani Barack Obama (kulia) amekaribishwa na Waziri mkuu Hailemariam Desalegn na mkewe (kushoto).
Alipowasili Ethiopia, Julai 26, 2015, rais wa Marekani Barack Obama (kulia) amekaribishwa na Waziri mkuu Hailemariam Desalegn na mkewe (kushoto)
Na RFI
Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Ethiopia Jumapili usiku katika ziara ya kikazi ya masaa 48. Ikiwa ni kwa mara ya kwanza rais wa Marekani kufanya ziara nchini Ethiopia, Barack Obama anaitambua Ethiopia kama mshirika muhimu katika vita dhidi ya ugaidi katika Pembe ya Afrika.
Hata hivyo Ethiopia ni nchi ambayo imeendelea kuvunja na kukiuka haki za binadamu.

Barack Obama yupo mjini Addis Ababa kwa muda wa siku mbili. Jumatatu asubuhi wiki hii, atakuwa na mazungumzo na Waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn, pamoja na rais Mulatu Teshome, ambaye ana majukumu ya kimfano.
Pamoja na ukuaji wake wa kiuchumi wenye kuvutia na raia wake zaidi ya milioni 90, Ethiopia kwa sasa imekua nchi yenye kuvutia barani Afrika. Suala la usalama litagubika mkutano kati ya Barack Obama na viongozi wa taifa hilo.(P.T)
Mkutano kuhusu hali inayojiri nchini Sudan Kusini na vita dhidi ya ugaidi unatazamiwa kuanza leo Jumatatu mchana. Wanamgambo wa kiislamu wa Al Shebab wamethibitisha kwamba wangeweza kuendesha mashambulizi na mikutano mbalimbali imeendelea kufanyika ili kupata ufumbuzi kwa vita vya wenyewe kwa vinavyoendelea kushuhudiwa nchini Sudan Kusini.
Hali hizi mbili ni zitajadiliwa zaidi katika mkutano huo unaosubiriwa kwa hamu na gamu Jumatatu wiki hii mchana katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa. Lakini kwa ujumla, eneo la Kaskazini Mashariki mwa Afrika bado linakabiliwa na vurugu ambapo Marekani bado ina washirika waaminifu. Ethiopia imewatuma wanajeshi wake kujiunga katika kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia, lakini pia katika mstari wa mbele katika upatanishi juu ya Sudan Kusini, na hivyo kuwa mshirika wa karibu wa Marekani.
Haki za binadamu katika mpango mbadala?
Kando na mikutano iliyopangwa, ziara ya Barack Obama inaweza pia kutafsiriwa kama ishara ya kuunga mkono utawala wa Ethiopia. Utawala ambao umeendelea kusalia madarakani kwa miaka mitano mfululizona kujipatia 100% ya viti Bungeni. Pia utawala ambao, mbinu inazotumia zimekua zikikosolewa na mashirika yanayotetea haki za binadamu nchini humo na kungineko duniani.
Katika mazingira haya, je rais wa Marekani atajitolea ili kuwapa nasaha viongozi wa nchi hiyo kuheshimu misingi ya demokrasia na uhuru wa kujieleza? Huenda akajizuia kutoa nasaha hiyo katika hotuba atakayoitoa mbele ya Umoja wa Afrika Jumanne wiki hii.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment