@nkupamah blog
Takriban watu 10 wameuawa katika mlipuko huo
Takriban watu 10 wameuawa kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea katika hoteli moja katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
Mwandishi
wa BBC katika mji huo anasema kuwa lori moja lilitumiwa kushambulia
hoteli ya Jazeera karibu na uwanja wa ndege wa taifa hilo.
Wajumbe wa kimataifa wamekuwa wakiishi katika hoteli hiyo ambayo imelengwa katika siku za nyuma.
Mlipuko mkubwa katika mkahawa maarufu Mogadishu
Ripota wetu anasema kuwa ni moja ya mashambulizi mabaya kuwahi kushuhudiwa mjini Mogadishu.
Anasema kuwa magari ya ambulansi yameanza kuokota miili.BBC
0 comments :
Post a Comment