Belle 9 haamini kama collabo zinaweza kumtoa kimataifa

Friday, July 24, 2015

Nkupamahmedia

Belle 9 amedai kuwa kwenye muziki wake haamini kama collabo ni njia sahihi ya kumfikisha kimataifa zaidi.

Akizungumza na mtandao huu, Belle amesema wapo wasanii kadhaa walioweza kutoboa bila hata kufanya collabo na wasanii wa mataifa ya nje.
 
“Mimi nimefanya collabo na Joh Makini, I am proud kwa sababu ni msanii mkubwa ambaye anafanya vizuri ndani na nje. Joh is too expensive sio simple tu kufanya naye collabo,” amesema Belle.
 
“Kama unavyojua msanii mkali hawezi kurekodi na msanii mbovu, mimi naamini inawezekana. Mimi naamini collabo sio kitu kinawezeka kunifikisha International, sijui wasanii wenzangu wengine. 
 
"Kwa sababu mtu kama Gsan alishiriki mpaka cipher ya BET najua sio kawaida, sasa Gsan alifanya collabo na nani? Na ni washkaji ambao walikuwa level kubwa. 
 
"Mimi siamini collabo inaweza kunifikisha huko, yaani siamini katika collabo kwa sababu ningekuwa nimeshafanya na nimesharelease. 
 
"Lakini najua collabo ni maisha ya muziki ambayo inatokea ukafanya lakini mimi sijafikiria nijaribu kufanya ndio nifike huko,” aliongeza muimbaji huyo.
 
Belle anajiandaa kuachia video ya wimbo wake ‘Shauri Zao’ iliyoongozwa na Hanscana.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment