Saturday, July 11, 2015
Nkupamah blog
Wapambe wa Mbunge wa Monduli Edward Lowassa hivi sasa wanafanya maandamano makubwa nje ya ofisi za CCM hapa makao makuu ya CCM wakipinga Mbunge huyo kuchujwa katika tano bora.
Wapambe hao wanaimba nyimbo mbalimbali za kukiponda chama cha Mapinduzi kwa madai kuwa chama hicho sio cha kindugu na pia sio cha kifalme.
Kwa namna nyingine hali si shwari hapa mkoani Dodoma ambapo sintofahamu imetawala kuhusiana na Edward Lowassa kukatwa.
Bado haijulikana nini hatma ya kikao kinachoendelea hivi sasa kwa kuwa wa wajumbe wengi wanapinga Lowassa kuchujwa.
Biashara zimesimama,makao makuu Dodoma.
Baadhi ya wapambe wa Lowassa wakipinga Kamati kuu kumchuja Lowassa.
Barabara zafungwa Polisi watanda kila kona kudhibiti usalama dhidi ya waandamanaji.
Wapambe wa Loawssa wakipinga kukatwa tano bora.
Nkupamah blog







0 comments :
Post a Comment