Lowasa kutangaza kuhamia CHADEMA Julai 26, Mwembe yanga ambako Dr Slaa alimtangaza kuwa Fisadi Papa...KAZI IPO!!

Zipo taarifa za uhakika kwamba Edward Lowasa, Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari Jumapili tarehe 26 Julai 2015 Jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kueleza mambo mengi juu ya mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM uliopelekea jina lake kukatwa.
Pia katika mkutano huo, Lowasa anatarajiwa kutangaza rasmi kujivua uanachama wake ndani ya CCM na kujiunga na CHADEMA ambapo baadaye jioni ataelekea viwanja vya Mwembeyanga ambako ataungana na viongozi wengine wa CHADEMA kwenye mkutano wa hadharaza. Mtakumbuka kuwa uwanja huo wa Mwembeyanga uliopo Temeke Dar es Salaam ulitumika kutaja orodha ya mafisadi 11 na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa mwaka 2007 ambapo jina la Lowasa lilikuwa miongoni mwa majina yaliyopo kwenye orodha hiyo.
Uamuzi wa Lowasa kwenda CHADEMA umetokana na kutimiza makubaliano ya kupeleka shilingi bilioni 10 ambapo fedha hizo zimekabidhiwa Jana Alhamis Tarehe 23 Julai 2015. Aliyekabidhi fedha hizo kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ni Apson Mwang'onda na makabidhiano yamefanyika kwenye Hotel ya Sea Cliff huku tukio hilo likishuhudiwa na Kingunge Ngombale Mwiru na wengine ambao sitawataja kutokana na sababu maalum.
Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa watu walioathirika na kukatwa kwa Lowasa hasa kutokana na fedha nyingi na muda kwa matumaini kuwa watakuwa "UPPER" baada ya Lowasa kushinda Urais. Miongoni mwao ni pamoja na Prof Juma Kapuya, Nazir Karamagi, Parseko Kone, Mgana Msindai, Kingunge Ngombale Mwiru, Mchungaji Gwajima, Andrew Chenge nk.
Hata hivyo, inadaiwa pia kuwa watu walio karibu na Lowasa akiwemo mfadhili wake mkuu Rostam Aziz ambaye amegoma kutoa fedha za kufadhili harakati za kwenda upinzani wanaendelea kumsihi kuwa asiende huko kwani atakuwa amejimaliza kabisa kisiasa. Pia inadaiwa kuwa mkewe Regina Lowasa amekuwa bitter sana na mpango wa mumewe kwenda upinzani na kwamba kwa siku kadhaa sasa amekuwa akiwafukuza wageni waliokuwa wanaenda nyumbani kwake hasa wale wa upinzani.
Credit:Thechoice.com
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment