SERIKALI KUITISHA KONGAMANO LA UWEKEZAJI WA BISHARA NDOGO NA ZA KATI

  • Written by  Nkupamahmedia
1.Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo) Zamaradi Kawawa akimtambulisha (kulia) Mkurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Diaspora, Rosemary Jairo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo),  Zamaradi  Kawawa  akimtambulisha (Mkurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Diaspora, Rosemary Jairo, (Kulia).
2.
Bi. Jairo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).(P.T)

3
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza.
SERIKALI kupitia Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kwa kushirikiana na  Kituo cha Uwekezaji cha Kimataifa (International Trade Centre Un-Agency), inatarajia kuitisha kongamano kubwa la aina yake likiwa na lengo la kuhamasisha ukuzaji wa biashara ndogo na za kati.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni jijini Dar, Mkurugenzi wa Idara ya Watanzania waishio nchi za nje katika Wizara ya Mambo ya Nje (Diaspora), Bi. Rosemary Jairo amesema, kongamano hilo litafanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar, kuanzia Agosti 13 – 15 mwaka huu.
Alisema, lengo kuu ni kuwahamasisha Watanzania waishio nje, kuwa na moyo wa kujitolea katika uendelezaji na ukuzaji wa biashara ndogo na za kati jambo ambalo kwa sasa linafanyika kwa kiwango na kasi duni. Pia, alisema kongamano hilo litahusisha Wizara za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ofisi ya Rais na Utawala Bora – Zanzibar na  Ofisi ya Waziri Mkuu.
Kikao hicho kinatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na  kufungwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.  Dkt. Ali Mohamed Shein.
Aliongeza, washiriki wa Diaspora katika kongamano hilo watapata fursa ya kufanya ziara visiwani Zanzibar kwa mwaliko maalum.
Habari / Picha: Na Denis Mtima / GPL.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment