TANESCO KANDA YA PWANI NA DAR YAWANASA WEZI SUGU WA UMEME 157


Published in Jamii
images
WATEJA wapatao 157 wamekamatwa na Shirika la ugavi wa umeme Tanesco Mkoa wa Pwani kwa kosa la kuiba umeme na kuhujumu miumndombinu kinyume cha sheria na taratibu na kupelekea
kulisababishia hasara shirika hili kiasi cha shilingi milioni 178 kutokana upotevu wa umeme ulitumika bila ya kulipiwa.
Kubainika kwa wezi hao wa umeme kumetokana na kufanyika kwa operesheni kabambe iliyofanywa na wakaguzi na maafisa mbali mbali kutoka kanda ya Dar es Salaam na Pwani na kukuta watu hao wanaiba nishati ya umeme kinymemela bila ya kufuata utaratibu.
Akizungumza na waandishi habari kuhusiana na wizi huo Mhandisi mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa mita na mdhibiti wa mapato kanda ya Pwani na Dar es Salaam Mrisho Sangiwa alisema kwamba kutokana na wizi huo kumefanya shirika hilo kupoteza kiasi kikubwa cha makusanyo ya mapato yao kutokana na vitendo vya wizi.
Sangiwa aongeza kuwa Tanesco kanda ya Dar es Salaam na Pwani wameamua kulivalia njuga suala hilo baada ya kugundua kuna baadi ya wateja wamekuwa wakifanya ujanja wa kuhujumu miumbombinu yao pamoja na kuiba hali ambayo inarudihs nyuma mipango waliyojiwekea katika kuboresha huduma ya nishati ya umeme kwa wateja wao.
“Zoezi hili tumeamua kuliendesha katika maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Pwani na msako huu lengo ikiwa ni kuwabaini wale wote ambao wamekuwa na tabia ya kuiba umeme na kuhujumu uchumi wan chi, hivyo kufanyika kw zoezi ii nin aimani kubwa kutaweza kupunguza kasi ya wizi wa umeme,”alisema Sangiwa.
Sangiwa alifafanua kwa sasa wateja ambao tayari wamewafanyia ukaguzi wa kuziangalia mita zao wanazidi 4200 ambao kati ya hao 157 ndio waliobainika wanaiba umeme kwa kijiunganishia kinymemela kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa maisha yao.
Naye Afisa usalama wa Shirika la umeme Tanesco Mkoa wa Pwani Henry Byarugaba akizungumzia kuhusina na mikakati waliyojiwekea katika kudhibiti wezi hao alisema kwamba wamejiwekea mikakati kabambe ya kufanya misako ya mara kwa mara nyumba hadi nyumba ili kuweza kuwabaini watu wachache ambao wanahujumu miundombinu ya Tanesco.
Afisa huyo alisema kwamba baada ya kumamatwa kwa wezi hao wa umeme kuna baadhi ya watu 26 tayari wameshafungulliwa mashitaka kwa kukutwa na makosa ya jinai ya kuhujumu miundombinu ya Shirika kinyume cha sheri na kwamba watachukulia hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Katika hatua nyingine Afisa usalama huyo amewatahadharia wananchi wa Mkoa wa Pwani na Taifa kwa ujumla kuwa makini na watu ambao wanajifanya ni wafanyakazi halali wa tanesco kumbe ni vishoka kitu ambacho amedai ni hatari .
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment