Wandishi wa Habari Wanawake watakiwa kujitokeza kugombea nafasi za Uongozi

images (5)
Wandishi wa Habari Wanawake wametakiwa  kujitokeza kugombania nafasi za Uongozi katika Chama cha Wandishi wa Habari  Zanzibar  (Zanzibar Press Club) ili waweze  kutoa mchango wao katika kukiendeleza Chama hicho.
 Hayo ameyasema Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari   Zanzibar Suzan Kunambi  wakati akizungumza na Mwandishi  wa habari hii  katika Ofisi ya Chma hicho  Kijangwani  Mjini Zanzibar.
Amesema  wanawake wanamchango mkubwa katika  kuimarisha maendeleo ndani ya  Vyama na Jumuia za Kiraia lakini wamekuwa hawajitokezi  katika kugombania nafasi za uongozi  na kupoteza fursa hiyo muhimu kwao.
Aidha ameelezea lengo la la kuanzishwa Chama cha Waandishi wa Habari Zanzibar  ni kuwaunganisha waandishi wa Habari pamoja ili waweze kuzitafutia ufumbuzi  changamoto zinzowakabili katika kazi zao za kila siku.
Amesema kuwa Chama hicho kimefanikiwa   kuwasaidia  wanachama wake kwa kuwapatia mafunzo  ya  muda mfupi ya uwandishi wa habari  yakiwemo kuandika habari za Biashara, Mazingira   na habari za Kimitandao .
Hata hivyo amezitaja baadhi ya changamoto zinazokabili chama hicho  kuwa ni pamoja na ukosefu wa  Fedha na Ofisi ya kudumu  ya kuendeshea shughuli zao na kuweza kujitegemea.       
Kunambi amewaomba waandishi  wa Habari  wa Zanzibar kujitokeza  kujiunga katika Chama hicho ili  kiweze kupata nguvu   na  kufikia  malengo  yaliyokusudiwa ya kuanzishwa kwake.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment