AFISA FEKI TRA ACHEZEA KICHAPO KISA HIKI HAPA

Nkupamah media

DAR ES SALAAM

Mtu mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja aliejifanya Afisa wa mamlaka ya mapato – TRA aliyekuwa na gari lenye namba za usajili T945  BYG amenusurika kifo mara baada ya kula kichapo
kutoka kwa wananchi wakati akiwa kwenye harakati za kufanya utapeli kwenye duka kubwa la VEW POINT lililopo Tabata Segerea jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa wafanyakazi wa duka hilo mtu huyo aliejifanya afisa kutoka mamlaka ya mapato TRA sio mara ya kwanza kufika eneo hilo kwani siku moja kabla  alifika akiwa na wenzake wawili na mmoja waliyemtambulisha kuwa ni mwandishi wa habari  na kufanikiwa kutapeli kiasi cha shilingi milioni tano.
Mtuhumiwa huyo sasa  amekamatwa na  kufikishwa kituo cha polisi Tabata Segerea kwa hatua zaidi za Kisheria.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment