Air France: Abiria 2 wakamatwa Paris

    Nkupamah media
    Abiria 2 wakamatwa Paris
    Maafisa wa polisi nchini Ufaransa wamewatia mbaroni mume na mkewe waliokuwa abiria katika ndege ya Air France iliyolazimika kutua kwa dharura nchini Kenya hapo jana kufuatia tishio la bomu ikiwa angani.
    Duru zinasema kuwa wawili hao ambao majina yao bado hayajatangazwa hadharani
    walikamatwa punde baada ya kutua katika uwanja wa kimataifa wa Charles de Gaulle.
    • Yamkini waliokamatwa ni afisa mmoja mstaafu wa polisi ambaye ni mshukiwa mkuu huku mkewe akitumika kama shahidi.
    • Mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege la Air France alifutilia mbali tahadhari ya' bomu' iliyosababisha ndege ya kutua Kenya kuwa ni bandia.
    Ndege hiyo ilikuwa na abiria 459 na wahudumu 14.
    Frederic Gagey aliwaambia waandishi wa habari mjini Paris Ufaransa kuwa kifaa kilichodhaniwa kuwa kilipuzi kilikuwa ni mbao na kisanduku cha karatasi tu wala hakikuwa na uwezo wowote wa kuhatarisha usalama wa ndege hiyo.
    Ndege hiyo ya Ufaransa chapa Boeing 777 nambari AF463 inayohudumu kati ya Mauritius na Paris ililazimika kutua baada ya kile kinachotajwa kuwa bomu bandia.
    Inasemekana kuwa abiria mmoja alikipata kifaa hicho chooni na akamfahamisha mhudumu mmoja wa ndege hiyo.
    • Ndege hiyo ilikuwa na abiria 459 na wahudumu 14.
    Mume na mkewe wamekamatwa walipotua mjini Paris
    Mhudumu huyo alimfahamisha rubani kuhusiana na kifaa hicho na shughuli za kutua kwa dharura zikaanza.
    Ndege hiyo ilitua saa sita usiku wa kuamkia Jumapili, huku wataalamu wa kutegua mabomu kutoka jeshi la wanamaji la Kenya wakiingia ndani ya ndege hiyo kukagua kifurushi kilicholeta taharuki.
    Sasa kitengo cha ujasusi cha Ufaransa kimeanzisha uchunguzi wa kina kubaini kilichosababisha tishio hilo.BBC
    Share on Google Plus

    About Unknown

    This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
      Blogger Comment
      Facebook Comment

    0 comments :

    Post a Comment