KATIKA
hali isiyo ya kawaida Mshereheshaji katika kinyang’anyiro cha kuwania
taji la Miss Universe Steve Harvey alijikuta akimpa wakati mgumu Miss
Colombia mara baada ya kutangaza kuwa alikosea kumtangaza mshindi wa
taji hilo.
Katika
tukio hilo ambalo limewaacha watu wengi vinywa wazi,lilishuhudia Steve
akimtaka radhi Miss Colombia na kumtangaza Miss Uphilipino kuwa ndiye
aliyekuwa anastahiki kushinda taji hilo kwa mujibu wa karatasi aliyokuwa
nayo ya matokeo ya mwisho.
Hata
hivyo haikumwia vigumu Miss Colombia kuvua taji hilo ambalo alikaa nalo
kwa muda usiozidi dakika tano kabla ya matokeo ya awali kubadilishwa
wakati akiwa katika harakati za kusherekea ushindi huo.
Muda
mfupi mara baada ya kuvuliwa taji hilo huku akiwa ameshika bendera ya
taifa lake alijikuta akitokwa na machozi mithili ya mvua hali iliyowapa
wakati mgumu washiriki wenzake na Steve kumbembeleza .
Je Ungekuwa ndiyo wewe ungefanyaje
Home
/
Uncategories
/
MC WA MISS UNIVERSE AJICHANGANYA NA KUMTAJA MSHINDI AMBAYE HAKUSTAHILI(VIDEO NA PICHAZZ)
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments :
Post a Comment