HOSPITALI YA MOUNT MERU INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA DAMU

60 
HOSPITAL ya mkoa wa Arusha, Mount Meru,inakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu salama  kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji damu kwa ajili ya matibabu yao.
Mganga mkuu wa hospital ya mkoa wa Arusha, Dakta Frida Mokiti, amekiambia kikao cha kamati ya maafa ya mkoa wa Arusha, kuwa hospital hiyo inahitaji uniti 1560 za damu salama,lakini  akiba ya damu salama iliyopo ni uniti 40 .
Kutokana na upungufu huo, mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Dakta Frida Mokiti, akatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujitolea damu nili kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanahitaji damu salama.
Amesema upungufu mkubwa wa adamu unasababisha wagonjwa wanaosubiri matibabu yanayotegemea damu salama kuwa kwenye   wakati mugumu ili kuokoa maisha yao.
Dakta Mokiti, amewaambia wajumbe wa kikao hicho cha kamati ya maafa ya mkoa kuwa makundi makubwa yenye uhitaji mkubwa wa damu salama kwenye matibabu yao ni  wajawazito, watoto na majeruhi .
Wajumbe wa kikao hicho ni pamoja na katibu tawala mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, wenye viti, madaktari wa wilaya na mkoa,sekretarieti ya mkoa,na wataalamu wa ngazi mbalimbali na maafisa afya .
 Dakta Mokiti,  amesema akiba ya damu salama iliyopo ni kidogo sana kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanahitaji damu nyingi,hivyo anaomba wananchi kujitokeza kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa.
Dakta, Mokiti, amesema mahitaji makubwa ya damu salama yanatokana na wingi wa wagonjwa wanaofika hospitalini hapo  hospital  kwa ajili ya matibabu yao,na pia hospital hiyo ya mkoa ndio inategemewa na hospital zingine kupata damu.
 Kwa upande wake kaimu katibu tawala wa mkoa huo,  Anza Amen Ndosa,aliwataka wakurugenzi wa haslmashauri za wilaya walifanyie kazi na wasitumie bajeti kama visingizio ili kukwepa jukumu la kuchangia damu salama kupita kwenye halmashauri zao.
Amesema uhai wa binadamu hautegeme bajeti bali damu hivyo  akazitaka halmashauri kuhamasisha wananchi kujitolea damu ili kuwezesha kupatikana akiba ya damu salama  ili kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanategemea damu.
Nae mwenyekiti wa  Chama cha msalaba mwekundu mkoa wa Arusha,Dakta Christopher Nzela, amekiambia kikao hicho kuwa Msalaba mwekundu,kimekuwa kikishiriki kuhamasisha wananchi kujitolea kuchangia damu salama kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa wanafikishwa vhospitalini kwa matibabu .
Hamasa hiyo inayotolewa na msalaba mwekundu, imekuwa ikisaidia kupatikana damu salama kutoka kwa wananchi wachache wanaojitokeza kujitolea damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa.
Nzera, amesema mwamko mdogo wa wananchi imekuwa ni changamnoto kubwa ya kufikia malengo ya upatikanaji wa damu salama na hilo linatokana na kuwa na uelewa mdogo na kutokujiamini kiafya.
Inawezekana wananchi walio wengi hawana uelewa wa kujitolea kuchngia damu salama,wengine hawajiamini hivyo wanakuwa na hofu ya damu zao kukutwa na maambukizi  ya virusi vya ugonjwa wa Ukimwi hivyo inakuwa vigumu kujitolea kutoa damu.
Nzera, amesema msalaba mwekundu mkoani Arusha,imekuwa ikihamasisha  vijana wa shule za sekondari na vyuo ambao huwa wanakuwa na mwamko mkubwa wa kujitolea damu salama,wakati makundi mengine ya kijamii yakiwa hayashiriki.

Malawi yafanya ziara ya kujifunza katika sekta ya Habari na Mawasiliano

x64
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel Akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi alimpomtembelea ofisini kwake Leo Jijini Dar es salaam.
x65 x66 x67 x68 x69
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel Akisalimiana na wageni toka Malawi walipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dar es salaam.
x70
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (Kushoto) Alizungumza na ujumbe toka Malawi (Hawapo pichani) walipomtembelea ofisi kwake leo Jijini Dar es salaam Kulia ni Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene.
x71
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi akiwa na ujumbe wake wakizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel walipomtembelea ofisi kwake leo.
x72
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel mwenye shati la batiki akizungumza na ujumbe toka Malawi walipomtembelea ofisini kwake leo.
x73
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel wa pili kutoka kushoto akizungumza na ugeni toka Malawi ofisi kwake leo kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi.
x74
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiagana na ujumbe uliomtembelea toka Malawi leo ofisini kwake.
x75
Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akifafanua jambo kwa ujumbe uliotembelea Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi.
x76
Baadhi ya maofisa wakuu  walioambatana na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi wakifatilia mazungumzo yaliyofanyika Wizarani hapo Leo.
x77
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi akifaafnua jambo kwa Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene walipokuwa wakizungumza kwenye mkutano uliofanyoka leo Jijini Dare s salaam.
x78
Mkurugenzi Msaidizi,sehemu ya Usajili wa Magezeti toka Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Raphael Hokororo akifafanua jambo kwa ujumbe toka Malawi uliotembela Wizarani hapo leo
x79
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utalii na Elimu toka Malawi Justin Adack Saidi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wake toka Malawi na na wakurugenzi wa Habari toka Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo kulia mwa Katibu mkuu huyo ni Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene
  picha Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment