TIMU YA JITEGEMEE FC YAUTWAAA UBINGWA WA MICHUANO YA KAWAMBWA CUP BAGAMOYO

2 (1)
TIMU ya soka ya Jitegemee Fc imewezwa kuutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Kawambwa Cup baada ya kuitandika  timu ya Buma Fc kwa  mabao 2-0 zote za Wilayani bagamoyo katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye uwanja wa Mwanakalenga mjini hapa.
 
Katika mchezo huo ambao ulihidhuliwa na umati mkubwa na mashabiki kutoka maeneo mbali mbali ya Bagamoyo na Jijini Dar es Salaam uliweza kuwavutia wengi kutokana na kila timu kuonyesha kandanda la kufundishika katika kipindi chote cha dakika 90 za mchezo huo.
 
Wachezaji wa timu ya Jitegemee Fc walianza mpira kwa kasi kwa kupeana pasi za kiufundi nakulisakama lango la wapinzani wao ambapo waliweza kuandika bao la kwanza kunako katika dakika ya 10 lililofungwa na mshambuiaji wao wa kutumainiwa Frank Raiko.
 
Kuingia kwa bao hilo kulionekana kuwachangannya wachezaji wa timu ya Buma fc na kujaribu kuelekeza mashambulizi yao ya kushitukiza lakini kutokana na safu ya ulinzi wa timu ya jitegemee kuwa imara waliweza kuzuia mashambulizi hayo.
 
Dakika ya 30 mchezji Yahaya Ramadhani aliweza kuwainua mashabiki wa timu yake ya Jitegemee baada ya kupachika bao la pili na kumwacha minda mlango wao Mbwana Matola akiwa ameduwaa na mpira huo kuzama nyavuni.
 
Hadi kipenga cha dakika 90 kinapulizwa timu ya Jitegemee Fc iliweza kuibuka kidedea kwa ushindi huo wa mabao 2-0 dhidi ya wapinzani wao na kutawazwa rasmi kuwa mabingwa katika mashindano hayo ya Kawambwa Cup kwa mwaka 2015.
 
Katika fainali za mchezo huo ambao ulihudhuriwa na katibu mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania i (TFF)Selestine Mwesigwa ambapo aliikabidhi timu ya Jitegemee zawadi ya kombe,seti ya jezi ,mipira miwili ,pikipiki na medali ya dhahabu .
 
Mshindi wa pili alikuwa ni Buma Mjini waliopatiwa seti ya jezi na mipira,na mshindi wa tatu timu ya Mwambao ilikabidhiwa seti ya jezi na mipira na  timu yenye nidhamu pamoja na kipa bora walipatiwa zawadi ya ngao .
Katibu Mwesigwa alimpongeza mbunge wa jimbo la Bagamoyo Dr Shukuru Kawambwa kwa kuandaa mashindano hayo kwa vijana kwa miaka kumi mfululizo  ambayo lengo lake kubwa alisema ni kukuza vipaji na kuwataka wabunge wengine nchini waweze kuiga mfano huo kama huo.
Kwa upande wake mwandaaji wa michuano hiyo Dr. Kawambwa aliwashukuru wadau wote walioshirikiana nae kufanikisha mashindano hayo na kusema kuwa mashindano hayo yamedumu kwa miaka 10 mfululizo ambapo ameahidi kuyaboresha na kuyaendeleza katika kipindi kingine cha miaka mitano ijayo. 
Kivumbi cha mashindano hayo ya Kawambwa Cup yalianza kutimua vumbi lake rasmi Novemba 24 ,ambapo jumla ya timu 73 kutoka kata saba za jimbo la Bagamoyo ziliweza kushiriki.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment