Waziri wa Nishati na Madini Prof.
Sospeter Muhongo (mbele) akiongoza kikao kilichoshirikisha watendaji wa
Wizara ya Nishati na Madini na kampuni ya Mtibwa Sugar Estates Ltd.
Profesa Muhongo aliitaka kampuni hiyo kuwekeza kwenye uzalishaji wa
umeme ili kukidhi mahitaji yake zaidi.
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akielezea mikakati na fursa zilizopo katika
sekta ya nishati.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtibwa
Sugar Estates Ltd, Nassor Seif akielezea shughuli zinazofanywa na
kampuni ya Mtibwa Sugar Estate Ltd.
……………………………………………………………………..
Na Greyson Mwase, Dar es salaam
Waziri wa Nishati na Madini
Profesa Sospeter Muhongo amewataka wawekezaji kutoka ndani na nje ya
nchi kujitokeza zaidi ili kuwekeza kwenye uzalishaji wa umeme nchini
lengo likiwa ni kufikisha megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025.
Profesa Muhongo aliyasema hayo
katika kikao chake kilichoshirikisha watendaji wa wizara ya nishati na
madini na kampuni ya kuzalisha sukari ya Mtibwa Sugar Estates
Limited.
Alisema kuwa lengo la serikali
ni kuhakikisha sekta ya nishati inachangia katika ukuaji wa uchumi wa
nchi kupitia uzalishaji wa umeme wa uhakika utakaopelekea ongezeko la
viwanda nchini.
Aliongeza kuwa ili nchi yoyote
duniani iweze kupiga hatua katika ukuaji wa uchumi wake, inahitaji umeme
wa uhakika na kusisitiza kuwa serikali inabuni vyanzo mbalimbali ili
kuhakikisha kuwa umeme wa uhakika unapatikana.
Aliendelea kusema kuwa ongezeko
la viwanda litapekelea ajira kuongezeka na uchumi kukua kuanzia
ngazi ya wilaya hadi nchi kwa ujumla.
Profesa Muhongo aliitaka
kampuni ya Mtibwa Sugar Estates Ltd kuwekeza kwenye uzalishaji wa umeme
zaidi na kuliuzia Shirika la Tanesco ili kupunguza tatizo la mgawo wa
umeme nchini.
Akielezea mikakati ya serikali
katika uimarishaji wa sekta ya umeme nchini, Profesa Muhongo alisema
kuwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) serikali imekuwa
ikiwaunganishia wananchi waishio vijijini umeme kupitia awamu tofauti
tofauti.


0 comments :
Post a Comment