Faiza wa ‘Sugu’ Aomba Radhi, Azindua Kipindi Chake

Nkupamah Media:

Faiza Ally
MSANII wa filamu nchini, Faiza Ally, amezindua kipindi cha runinga kiitwacho ‘Stars’ ambacho kitakuwa kikizungumzia maisha yake.

Akizungumza katika kipindi cha Friday night live kinachoongozwa na mtangazaji, Sami Misago, wakati akitambulisha kipindi hicho alisema kitaanza kuoneshwa Jumanne katika kituo cha Eatv na kitahusu maisha yake ya kila siku.

“Kipindi changu kipya kitakuwa kikiitwa ‘Stars’ na kitakuwa kikizungumzia maisha yangu ya kila siku, nataka watu waone upande wangu mwingine kwa sababu kitu mnachokiona kina utofauti mkubwa na maisha yenu, kwa hiyo nataka kuonyesha watu kuna maisha tofauti na yale ambayo wanayaona,” alisema Faiza.

Msanii huyo alitumia fursa hiyo kuwaomba radhi mashabiki wake baada ya siku chache zilizopita kutuma video ya mwanawe, Sasha iliyomwonyesha akiomba fedha za kusuka huku akilia hali ambayo ilitafsiriwa kuwa ni udhalilishaji kwa mtoto huyo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment