Baada
ya jana, jumatatu kuwepo kwa taarifa kuwa Manchester United ipo tayari
kulipa kiasi cha Pauni Milioni 60 kwa ajili ya kupata saini ya staa wa
Gabon na klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani, Pierre-Emerick
Aubameyang, leo imetoka stori nyingine kuhusu usajili wa mchezaji huyo.
Kwa
mujibu wa mtandao wa Daily Mirror umeripoti kuwa Manchester United ipo
tayari kumlipa Aubameyang mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki pindi
atakatua kwenye klabu hiyo ya Uingereza.
Mtandao
huo umeripoti kuwa uhamisho wa Aubameyang unauwezekano mkubwa
kukamilika baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa wawakilishi wa Aubameyang
wameshakutana na viongozi wa Man United ili kujadili uhamisho huo.
Aubameyang,
26 kwa msimu wa 2015/2016 ameshaifungia klabu yake ya Dortmund magoli
30 na hivyo kuzivutia klabu mbalimbali barani Ulaya ikiwepo Arsenal ili
kupata saini ya mchezaji huyo bora Afrika, 2015.


0 comments :
Post a Comment