NRA kushiriki uchaguzi wa marudio Zanzibar

IMG_3275
Hassan Almasi Kisabya Katibu Mkuu wa Chama cha NRA Bara akitoa msimamo wa chama hicho kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi wa marudia Zanzibar utakaofanyika Machi 20 mwaka huu  kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Leo jijini Dar es salaam , katikati ni  Mussa Limamu Mketola Makamu Mwenyekiti Baraza la Wazee NRA  na kushoto ni Janken Malik Kasambara  Afisa Habari wa Chama cha NRA. Nkupamah media:
…………………………………………………………………………………………………………
Na Nyakongo Manyama MAELEZO
Chama Cha National Reconstruction Alliance (NRA) kutoka Zanzibar  kimethibitisha kushiriki uchaguzi wa marudio wa Zanzibar unaotarajiwa kufanyika Machi 20, mwaka huu baada ya kikao kilichofanyika Februari 15.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Tanzania Bara Hassan Almasi Kisabya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam ambapo amesema kuwa Chama hicho kitashiriki uchaguzi wa marudio na kusisitiza kuwa tamko lililotolewa na mgombea wao la kutoshiriki uchaguzi wa marudio lipuuzwe kwani ni tamko lake binafsi na sio msimamo wa chama.
“Tamko lililotolewa tarehe 14/02/2016 Si Tamko la chama cha NRA bali ni tamko binafsi na wale waliomuagiza kwani yeye hana mamlaka ya kukisemea chama wala wagombea wengine wa chama pasipo Baraka na vikao halali vya chama” alisema Kisabya.
Amesisitiza  kuwa maamuzi ya chama ni sharti yatoke katika chama na sio kwa mgombea na ikiwa yeye amejitoa anatakiwa afuate taratibu za kisheria katika kujitoa kama alivyofuata sheria katika kugombea nafasi hiyo.
Aidha, Chama kinatoa taarifa kwa wagombea wote Zanzibar kujiandaa na wapiga kura kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, mwaka huu ili kutimiza haki yao kikatiba na kuchagua viongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano ijayo
Chama cha NRA ni miongoni mwa vyama 14 vilivyosimamisha wagombea katika uchaguzi wa  Oktoba 25 mwaka jana katika Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofutwa kwa nafasi ya Rais.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment