Baada ya kuwepo kwa maneno mbalimbali ambayo yalikuwa yakizunguzwa hatimaye Rais Dkt. John Pombe Magufuli amezungumzia uchaguzi mkuu wa Meya wa Dar es Salaam.
Rais Magufuli amezungumzia uchaguzi huo wakati alipokuwa akitekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda la kutaka kuhakikiwa kwa silaha zote zinazomilikiwa na wananchi ambapo yeye amehakikiwa silaha anazomiliki ambazo ni Shortgun na Pisto.
Ili kufanyika kwa uchaguzi huo Dkt. Magufuli amezitaka pande zote ambazo zinagombea kiti cha umeya wa jiji la Dar es Salaam, kukamilisha mchakato wa kumpata meya katika uchaguzi uliopangwa kufanyika kesho Machi, 22 badala ya kuendelea kurumbana.
Dkt. Magufuli amesema kuwa upande wowote uwe tayari kupokea matokeo ya uchaguzi huo, ili meya apatikane na jiji liweze kuendelea na mipango yake ya kuwahudumia wananchi bila vikwazo.
“Mahali tunapostahili kushinda kama tunashinda tushinde kweli, lakini mahali tunaposhindwa napo tukubali kushindwa, na hiyo ndiyo demokrasia ya kweli,” amesema Dkt. Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amezungumzia zoezi la uhakiki wa silaha na kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Jeshi la Polisi kwa kuanzisha zoezi hilo na kuwataka wamiliki wa silaha nchi nchi nzima kuhakikisha wanahakiki silaha wanazomiliki.
Pia amelitaka Jeshi la Polisi kuongeza juhudi ili kukabiliana na watu wanaojihusisha na vitendo vya uharifu ili kutokomeza kabisa vitendo hivyo.
“Ni aibu kumuona askari polisi mwenye silaha ananyang’anywa silaha, ni aibu na nasema hiyo ni aibu, mpaka jambazi akunyang’anye silaha na wewe una silaha,” amesema Rais Magufuli.
Kwa upande wa Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro, amemshukuru Rais Magufuli kwa kuunga mkono zoezi hilo na amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa uhakika.
227143f1-4d6c-42ee-8ea1-90f9fa86d78b
20160321053640
d030fc7a-4c03-417f-b28f-d9f1d9ef5717
e7e04467-4a74-4728-b7eb-d85c2957dcfe