Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imeendelea leo kwa michezo minne kupigwa katika viwanja mbalimbali nchini.
Matokeo ya michezo hiyo Simba imeendelea kujichimbia kileleni baada ya kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila dhidi ya Tanzania Prisons, goli lililofungwa na Awadh Juma katika dakika ya 88 na hivyo kufikisha alama 54 ikiwaacha Yanga kwa alama nne.
Matokeo kamili ni;
Simba 1 – 0 Tanzania Prisons
Mgambo Shooting 1 – 1 Mwadui FC
Majimaji 1 – 0 Stand United
Kagera Sugar 3 – 0 Coastal United