MBOWE AITWA MBEYA HARAKA KUTATUA MGOGORO WA CHAMA

Nkupamah media:

Wajumbe wa mkutano mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo, CHADEMA,wilaya ya mbeya mjini wamemtaka mwenyekiti wa chama hicho taifa,Fremman Mbowe kwenda haraka jijini Mbeya kutatua mgogoro wa kiuongozi unaoendelea ndani ya chama kabla haujaleta madhara makubwa na kusababisha chama hicho kupoteza imani kwa wananchi.

Tamko la wajumbe hao wa mkutano mkuu wa Chadema wilaya ya Mbeya mjini linatokana na kikao cha ambacho kilifanyika hivi karibuni chini ya usimamizi wa makamu mwenyekiti wa Chadema taifa upande wa Zanzibar,Mohamed Issa Mohamed kilichoamua kuvunja kamati ya utendaji ya chama hicho wilaya ya Mbeya mjini na kuweka uongozi wa muda, jambo ambalo linapingwa vikali na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho.

Kutokana na hatua hiyo baadhi ya wajumbe wa mkutano huo wakadai kuwa wao hawautambui uongozi wa muda uliowekwa na badala yake wataendelea kuwatambua viongozi waliowachagua kikatiba.

Akitoa tamko la pamoja, katibu wa mkutano huo,Hezron Edwin Mwaisengela amesema kuwa wajumbe wanamtaka mwenyekiti wa chama taifa kufika mbeya haraka ili kutatua mgogoro huo kwa maslahi mapana ya chama.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment