Mwanaharakati ashikiliwa na Polisi kwa kufanya vurugu kwenye mkutano wa mbunge


Jeshi la Polisi wilayani Mkalama, Mkoani Singida linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Iguguno, Tarafa ya Kinyangiri, maarufu kwa jina la “Mwanaharakati”kwa tuhuma za kufanya vurugu kwenye mkutano wa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki(CCM), Allani Joseph Kiula.
Tukio la kufanyika kwa vurugu hizo lilianza kujitokeza tangu mkutano huo ulipoanza majira ya saa kumi jioni kwenye ofisi za afisa mtendaji wa kata ya Iguguno ambapo idadi kubwa ya wananchi wa kijiji hicho pamoja na vijiji vinavyokizunguka walihudhuria kumsikiliza mbunge wao aliyekwenda kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mwakilishi wao.
Hata hivyo mwanaharakati huyo ambaye kwa muda mwingi alionekana kutoa kauli za kejeli kwa mbunge huyo kwa sauti kali na ya juu,wakati wananchi wakimsikiliza mwakilishi wao aliyewatembelea kwa mara ya kwanza kuwashukuru na kusikiliza baadhi ya kero zinazowakabili.
Ilikuwa ni muda wa saa 11:00 za jioni wakati ulipowadia muda wa maswali na majibu kutoka kwa mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki, ndipo Muna alipoinua mkono kuomba nafasi ya kuuliza maswali matatu kwa mbunge wao huyo.
“Naitwa Joseph Luther Muna “Mwanaharakati asante sana mwenyekiti, asante sana mbunge na asante sana wageni mimi nina maswali matatu namshukuru sana mbunge amesema kwamba mkutano wa kutatua kero…ndipo ghafla mbunge alimtaka mwanaharakati huyo kuuliza swali badala ya kutoa maelezo marefu kwa kuokoa muda,” alieleza shuhuda wa tukio hilo na kuongeza.
“Akawa anazomewa na wananchi waliohudhuria mkutano huo, mwanaharakati huyo alianza kwa swali la kwanza kwa kuuliza kuwa mkuu wa wilaya alikuja tarehe 2, alipokuja alichukua kero 16 na siyo kero 20 kama unavyodai wewe”
Katika swali lake hilo Muna maarufu mwanaharakati aliweka wazi kuwa katika hizo kero 16 na mbunge ni kero hivyo ni kwa nini asingesubiri kero hizo zishughulikiwe na mkuu wa wilaya ili ijulikane zitatatuliwa vipi badala ya yeye kusema anakwenda kuzishughulikia kero hizo.
Baada ya maelezo yake hayo aliyokuwa akidai kuwa ni swali, wananchi kwa pamoja waliohudhuria mkutano huo walijitokeza na kusisitiza kwamba Muna hakuwa na swali la msingi zaidi ya ubabaishaji tu mkutanoni hapo na waliendelea kumzomea kwa kitendo cha kupoteza nafasi kwa wengine waliokuwa na maswali.
“Mheshimiwa mbunge ulipokwenda bungeni tangu uliporudi kutoka bungenihaujatupatia mrejesho zaidi ya leo kusema kwamba unachomoa kero zako ili tuone kuwa wewe huna kero unazotukwaza,kwa nini haujatupa mrejesho wa bungeni kwanza ndipo uingie katika kutatua kero zetu,” alihoji mwanaharakati huyo.
Hata baada ya kumaliza kuuliza maswali hayo mwanaharakati huyo alianza kutoa lugha chafu kwa mbunge wa jimbo hilo wakati aliposimama akijibu maswali ya wananchi,jambo lililowafanya Jeshi la Polisi kuchukua hatua za kumkamata na kumpeleka kituoni kwa tuhuma za kufanya fujo mkutanoni.
Mtuhumiwa wa tuhuma hizo amewekwa katika kituo kidogo cha Polisi cha kata ya Iguguno akisubiri zaidi hatua za kisheria zaidi.
Na Jumbe Ismailly, Mkalama
DSCN0030Katibu wa CCM wilaya ya Mkalama,Bi Ernestina (wa pili kutoka kushoto aliyevaa fulana ya njano) akisikiliza kwa makini kero za wananchi wa kata ya Iguguno wakati wa mkutano wa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki(CCM), Bwana Allani Kiula
DSCN0019Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa mbuge wa jimbo la Iramba mashariki(CCM)Bwana Allani Kiula alipokwenda kutoa shukurani kwa wananchi hao pamoja na kupokea kero zao. 
DSCN0037Askari wa jeshi la polisi katika Kituo kidogo cha Mji mdogo wa Iguguno(aliyevaa sare za jeshi la polisi) akiwa katika mkutano wa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki(CCM)Bwana Allani Kiula akisimamia ulinzi katika kipindi chote cha mkutano na kuwachukulia hatua watu wenye nia ya kuvuruga mkutano huo.
DSCN0057Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa mbuge wa jimbo la Iramba mashariki(CCM)Bwana Allani Kiula
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment