Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina Kulia Akifyeka, katika Mtaa wa TPDC Mikocheni Jijini Dar es Salam leo kutekeleza agizo la Mh. Raisi la kufanya usafi, ambapo serikali imetenga kila Jumamosi ya mwisho wa Mwezi kuwa siku maalum ya usafi.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina, akifanya usafi katika mtaro wa maji machafu katika mtaa wa TPDC, maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa siku ya usafi jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Kulia Bi Blandika Cheche Afisa Mazingira mkuu, na katikati Mkururugenzi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC Bw. Boniventure Baya wakifanya usafi kwa pamoja katika mtaa wa TPDC, Mikocheni Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la serikali, la kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi la kufanya usafi wa mazingira.
Aliyevaa shati ya blue Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira mh Luhaga Mpina akiweka taka katika gari la kuzolea taka katika mtaa wa TPDC Mikocheni JIjini Dar es salaam leo, Jumamosi ya mwisho wa Mwezi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Serikali la usafi wa Mazingira .
(Picha zote na Evelyn Mkokoi wa Makamu wa Rais)
0 comments :
Post a Comment