Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ataka usafirishaji Haramu wa Madini Udhibitiwe


WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kudhibiti usafirishaji haramu wa madini ya bati, akieleza kuwa yuko mwanamke ambaye si rais wa Tanzania anayesafirisha kinyume cha utaratibu.

Alitaka kujua hatua zilizochukuliwa kudhibiti hali hiyo na kumhoji Mkuu wa Wilaya, Benedict Lenga endapo anafahamu watu wanaosindikiza wezi hao wa madini.

“Madini ni tija, lazima tujue yanasafirishwa kwa kigezo kipi.Tunajua wakati mwingine tunasindikiza watu wanaoiba madini yetu,” alisema Majaliwa na kuhoji endapo Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ndiye anayesindikiza. Hata hivyo, alijibiwa kuwa hahusiki.

Aidha, alimtaka Lenga na watu wake waimarishe ulinzi ili biashara hiyo ya madini idhibitiwe. Majaliwa alikuwa akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, John Mongella, alipowasili hapa jana kuanza ziara ya siku nne.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment