Makala Awavalia Njuga Watumishi HEWA Jijini Mbeya



Timu ya watu 16 imeundwa ili kuhakiki upya watumishi hewa katika halmashauri zote mkoani Mbeya, lengo likiwa ni kujiridhisha.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amesema kwenye uzinduzi wa mradi wa uimarishaji mifumo ya sekta za umma kutokana na kuwapo kwa tatizo la watumishi hewa.
 
“Rais alituagiza kuhakiki watumishi wote na ikafanyika hivyo, lakini kutokana na kuwapo kwa udanganyifu nimeunda timu ambayo imeanza kazi jana (juzi) kuhakiki upya watumishi ili kujiridhisha na kupata ukweli wa watumishi wetu,” amesema.
 
Makalla amesema timu hiyo imegawanyika katika makundi mawili na kwamba, wajumbe wanatoka idara mbalimbali za Serikali wakiwamo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru)
Share on Google Plus

About mtilah

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment