Baada
ya jana Jumatano Afisa Habari wa Yanga, Jerry Muro kuwaomba wapinzani
wao Simba kuwashangilia katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi
ya Al Ahly, wapinzani wao Simba wamezungumzia ombi hilo.
Akizungumza
na E Fm katika kipindi cha E Sports, Simba kupitia kwa msemaji wake,
Haji Manara wamesema wao hawawezi kuwaambia mashabiki wao kuwashangalia
Yanga au kuacha kuwashangilia.
Manara
amesema mashabiki wa Simba wataenda uwanjani kuangalia mpira kama
mashabiki wengine na maamuzi ya kushangilia mchezo huo ni uamuzi wao
wenyewe.
“Mimi
siwezi kuwaambia washangilie Simba au waache kuwashangilia wataenda
kutazama mpira kama mashabiki wa soka nchini na wataamua wenyewe wakae
upande upi,” amesema Manara.
Aidha
ameongeza kuwa anashangazwa na kitendo cha Muro kuwaomba kuishangilia
Yanga kwani kwa miaka iliyopita Simba ilipokuwa na michezo ya kimataifa
walikataa kuwasapoti na kutolea mfano mchezo wa TP Mazembe uliochezwa
uwanja wa Taifa Dar es Salaam na kuwepo tuhuma kuwa mashabiki wa Yanga
walivaa jezi za Mazembe na kuishangilia.


0 comments :
Post a Comment