Golikipa
wa Barcelona, Marc-Andre ter Stegan amekanusha uvumi ulikuwa umesambaa
kuwa amesaini mkataba na Manchester City na kueleza atazungumza hatma
yake baada ya msimu kumalizika.
Akizungumza
na kituo cha redio cha Al Primer Toque alisema hakuna dili lolote na
Mnchester City nakwa sasa anachoangalia ni kucheza vizuri na kuona timu
yake ikishinda michezo yake.
“Sio
kweli kuwa nimesaini Manchester City … mwishoni kwa msimu tutaangalia
hali jinsi ilivyo ndipo nitazungumza tena, sawa? Tuna michezo mingi kwa
sasa na hilo ndiyo pekee naweza kusema kwa sasa,
“Kwa
mimi jambo muhimu ni kucheza vyema na tushinde michezo yetu yote.
Barcelona ni timu kubwa, siwezi kusema zaidi, tutaona jinsi itakuwa,”
alisema


0 comments :
Post a Comment