Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au 
kulipa faini ya Sh4.5 milioni, mfanyabiashara Huifang Ma baada ya 
kupatikana na hatia ya kuuza bidhaa na kushindwa kutoa risiti kwa 
kutumia mashine ya kieletroniki. 
Ma ambaye ni raia wa China na mkazi
 wa Mtaa wa Narung’ombe eneo la Kariakoo, alihukumiwa kifungo hicho 
baada ya kukiri mashtaka mawili yaliyokuwa yakimkabili likiwamo la 
kushindwa kujisajili kulipa kodi ya ongezeko la thamani (Vat). 
Akisoma
 hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mwanadamizi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Said 
Mkasiwa alisema kwa kuwa mshtakiwa alikiri mashtaka yanayomkabili, 
anatakiwa kulipa faini au kwenda jela miaka mitatu. Hata hivyo, Ma 
alilipa faini na kuachiwa huru. 
Katika hati ya mashtaka, ilidaiwa 
kuwa Machi 23, mwaka huu eneo la Karikaoo, mshtakiwa alishindwa kutoa 
risiti za kieletroniki kwa mteja wake. 
Ilidaiwa kuwa siku hiyo 
mshtakiwa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya HM Textile Co Ltd iliyopo Mtaa
 wa Agrey, Kariakoo, alishindwa kutumia mashine za EFDs kwa ajili ya 
kutoa risiti kwa wateja walionunua bidhaa dukani kwake.
Kosa la pili, mshtakiwa alishindwa kujisajili kama mlipa kodi wakati akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria. 



0 comments :
Post a Comment