Mkuu
wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Joshua Msuya, amewahimiza waandishi wa
habari kufanya kazi kwa karibu na TAKUKURU,ili kuharakisha kukomesha
vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ikiwa ni kuunga mkono dhamira ya
serikali ya awamu ya tano ya kukomesha vitendo hivyo.
Msuya
ametoa wito huo leo wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji ya
kipindi cha mwaka jana mbele ya waandishi wa habari katika kikao kifupi
kilichofanyika ofisini kwake.
Alisema
kila Mtanzania ni shuhuda mzuri kwamba serikali ya rais Dk.Magufuli
imedhamiria kwa dhati kukomesha vitendo viovu vya kuomba na kupokea
rushwa,ili wananchi waweze kupata haki zao za msingi bila kuzinunua
kupitia vitendo vya rushwa.
“Kama
mnavyofahamu kwamba jukumu la kukomesha vitendo vya rushwa sio la
TAKUKURU peke yake,ni letu sote na ninyi waandishi wa habari
mkiwemo.Tumieni taaluma yenu kufichua vitendo hivi vya kuomba na kupokea
rushwa,ili mamlaka husika ziweze kuchukua hatua ya
kuvikomesha”,alifafanua Msuya.
Mkuu
wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Joshua Msuya, akitoa taarifa yake ya
utekelezaji kwa mwaka jana mbele ya waandishi wa habari. Msuya alisema
kwa mwaka jana (2015) walipokea taarifa ya vitendo vya kuomba na kupokea
rushwa 44 na kudai kuwa TAMISEMI imeongoza kwa kulalamikiwa kwa matukio
15. Kulia ni Mkaguzi wa miradi ya serikali kanda ya kati, Domina
Mukama.
Katika
hatua nyingine, Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani hapa,alisema katika
kipindi cha mwaka jana,walipokea taarifa 44 za malalamiko dhidi ya
vitendo vya kuomba na kupokea rushwa.
“Idara
zinazoongoza kwa kulalamikiwa ni kutoka TAMISEMI..watendaji wa kata na
vijiji malamamiko 15,halmashauri na manispaa 14,jeshi la polisi
malalamiko saba na wengineo nane”,alisema.
Aidha,Msuya
alisema jumla ya kesi mbili zimeishafikishwa mahakamani mwaka jana, na
kesi zingine 11 zinaendelea kusikilizwa, wakati miradi ya maendeleo
ipatayo 30, imekaguliwa.
Kuhusu
kudhibiti vitendo vya rushwa katika kipindi hicho, alisema kuwa
walichukua hatua mbalimbali ikiwemo na kuchambua mifumo yenye harufu ya
rushwa na wametoa elimu juu ya madhara ya rushwa kwenye washara na
semina mbalimbali.
Baadhi
ya waandishi wa habari mjini Singida, wakimsikiliza Mkuu wa TAKUKURU
mkoa wa Singida, Joshua Msuya, wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji
kwa kipindi cha mwaka jana.Amedai jumla ya matukio 44 yaliripotiwa na
TAMISEMI iliongoza kwa malalamiko 15.
Pia alisema wataendelea
kuwaelimisha wananchi wasitoe rushwa kwa mtu ye yote mtoa huduma bali
watoe taarifa za vitendo vya kuombwa hongo mapema iwezekanavyo.
Akisisitiza, alisema TAKUKURU mkoa inatoa wito kwa wananchi wote kwa ujumla,kujiepusha na vitendo vya rushwa na kushiriki kikamilifu kutoa taarifa za vitendo vya rushwa pale wanapobaini kutokea/kutaka kutokea kwa vitendo vya rushwa.Vile vile watoe ushirikiano kwenye uchunguzi na kushiriki kutoa ushahidi mahakamani pale watakapohitajika kufanya hivyo.
Wakati huo huo,Msuya amewataka watumishi wote wa idara za serikali,taasisi na mashirika yote ya umma wazingatie sheria,kanuni na taratibu za kazi.Wale wote watakao jihusisha na vitendo vya rushwa,sheria kali itachukua mkondo wake.
Akisisitiza, alisema TAKUKURU mkoa inatoa wito kwa wananchi wote kwa ujumla,kujiepusha na vitendo vya rushwa na kushiriki kikamilifu kutoa taarifa za vitendo vya rushwa pale wanapobaini kutokea/kutaka kutokea kwa vitendo vya rushwa.Vile vile watoe ushirikiano kwenye uchunguzi na kushiriki kutoa ushahidi mahakamani pale watakapohitajika kufanya hivyo.
Wakati huo huo,Msuya amewataka watumishi wote wa idara za serikali,taasisi na mashirika yote ya umma wazingatie sheria,kanuni na taratibu za kazi.Wale wote watakao jihusisha na vitendo vya rushwa,sheria kali itachukua mkondo wake.
Jengo la ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Singida.(Picha na Nathaniel Limu).


0 comments :
Post a Comment