Mohammed Dewji ‘MO’ afunguka ya moyoni kuhusu Simba, Mwana FA naye atoa maoni yake kwa uongozi

Michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imemalizika hapo jana na Simba SC ikijikuta ikiangukia nafasi ya tatu baada ya kupokea kichapo cha goli 2-1 kutoka kwa JKT Ruvu na hivyo kusalia na alama 62 huku Azam wakifikisha alama 64 na kushika nafasi ya pili baada ya kutoa sare ya goli 1-1 na Mgambo JKT, shabiki wa damu wa Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ ameamua kufunguka yaliyo moyoni mwake kutokana na matokeo hayo.
Mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Simba na JKT Ruvu, MO ambaye pia ni Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL Group) alitoa yaliyo moyoni kwake kuhusu Simb kupitia ukurasa wake wa Twitter, ujumbe ambao ulionekana kuwagusa mashabiki wa Simba na wadau wengine wa michezo nchini.
MO aliandika “#Simba mnatunyima raha, tumechoka kutaniwa na kutukanwa mitaani”
Aidha mashabiki wa Simba na wadau wa michezo nchini hawakuwa nyuma kutoa na wao maoni yao kuhusu mwendendo wa Simba.
Wakati MO akiandika hayo, Mwana FA ambaye naye ni shabiki wa Simba SC aliandika ujumbe ambao ulionekana kuwa na maumivu na kuwatumia ujumbe viongozi wa klabu hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment