HILLARY CLINTON ATIMIZA IDADI ANAYOPASWA

Hilarry Clinton uso kwa uso na Donald Trump
Hillary Clinton ameripotiwa kufikisha idadi ya wajumbe anayohitaji ili kupata uteuzi wa chama chake ya kuwania nafasi ya urais wa Marekani.
Idadi hiyo imefikiwa katika majumuisho yanayofanywa na wakala wa habari Associated Press.
Taarifa hizi zinakuja kabla ya kinyang'anyiro cha leo katika majimbo sita, ikiwemo California.
AP imesema idadi hiyo imefikiwa baada ya ushindi wa Clinton dhidi ya mshindani wake Bernie Sanders huko Puerto Rico mwishoni mwa juma na kuongezeka kwa idadi ya wajumbe ambao wanaruhusiwa kumuunga mkono mtu yeyote wanaemtaka.BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment