Rais Magufuli Amuapisha Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Juni, 2016 amemuapisha Mhe. Gerson John Mdemu kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Gerson John Mdemu alikuwa Karani wa Baraza la Mawaziri (Cabinet Clerk)
 
Mhe. Gerson John Mdemu amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Dkt. Tulia Ackson ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
04 Juni, 2016

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment