Baada
ya kutolewa katika mashindano ya Uefa Euro 2016 na kocha wa timu ya
taifa ya Uingereza, Roy Hodgson kuchukua uamuzi wa kujiuzulu kuifundisha
timu hiyo, nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza, Wayne Rooney
amejitokeza na kutoa maoni yake kuhusu kocha ambaye wa kuifundisha timu
hiyo.
Rooney
alisema kuwa ni jambo sahihi nafasi hiyo akipatiwa kocha Mwingereza
ambaye ana uwezo mkubwa wa kufundisha soka na atakayeweza kuisaidia timu
ya taifa hilo kufanikiwa kisoka.
“Anatakiwa
kuwa na uwezo wa ziada ili aifanye kazi yake vizuri, awe Mwingereza au
siyo lakini tusubiri na kuona, nadhani anatakiwa kuwa mtu ambaye
anautaifa na ambaye ni mtu bora,
“Nadhani
itakuwa sahihi kama akiwa Mwingereza, ni sahihi awe Mwingereza lakini
ambaye atakuwa ni sahihi kwa kazi hiyo,” alisema Rooney.


Blogger Comment
Facebook Comment