Wawakiishi
pekee wa Tanzania katika mashindano ya kimataifa, Dar Young Africans
imecheza mchezo wake wa pili wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho
la CAF dhidi ya TP Mazembe ya Congo DRC na kukubali kichapo cha goli
moja kwa bila.
Yanga
ambayo ilifanya maandalizi kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuweka
kambi Uturuki na kuwaruhusu mashabiki wa soka nchini kutizama mchezo huo
bure katika uwanja wa Taifa, ilianza mchezo huo dhidi ya TP Mazembe kwa
kasi lakini ilishindwa kutumia vyema nafasi zilizotengenezwa.
Kipindi
cha pili TP Mazembe walionekana kubadilika na kuanza kufanya
mashambilizi machache katika lango la Yanga na katika dakika ya 75
walifanikiwa kupata goli kupitia mchezaji wake, Merveille Bope baada ya
kupigwa faulo fupi karibu na lango la Yanga, goli lililodumu hadi mchezo
huo unamalizika.
Kwa
matokeo hayo, Yanga sasa imepoteza michezo yake yote miwili baada ya
wiki iliyopita kufungwa goli moja kwa bila na Mo Bejaia ya Algeria na
leo kupoteza mchezo wa pili dhidi TP Mazembe.
Mchezo unaofuatia wa Yanga unataraji kuwa dhidi ya Medeama mchezo utakaochezwa Julai, 15.


Blogger Comment
Facebook Comment