MAJAMBAZI
wanne wamevamia kijiji cha Benaco kilichopo katika Wilaya ya Ngara
mkoani Kagera kwa muda wa saa tatu ambapo wamefanikiwa kupora Sh milioni
2.4 na simu ambazo hazikujulikana idadi yake kwa mfanyabiashara mmoja
wa huduma ya M-Pesa.
Kaimu
kamanda wa polisi mkoa wa Kagera ambaye pia ni ofisa upelelezi wa
polisi mkoa huo, Abel Mtagwa, alisema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa
kuamkia jana ambapo majambazi hao walikuwa na silaha moja ya kivita
aina ya SMG.
Alisema
kuwa wakati majambazi wakijiandaa kuondoka eneo hilo walimpiga risasi
mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Gankabo
Wilayani Kibondo mkoani Kigoma aliyetambuliwa kwa jina la Nelson Simon
(15) na kumjeruhi mguu wake wa kulia. Mwanafunzi huo amelazwa katika
hospitali teule ya Murgwanza iliyopo wilayani humo.



Blogger Comment
Facebook Comment