VIDEO: Mourinho aanza kibarua kwa ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Wigan, magoli yote yapo hapa




Safari ya kibarua cha kocha mpya wa Manchester United, Jose Mourinho imeanza kwa mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na msimu mpya wa 2016/2017 dhidi ya Wigan Athletic kwa ushindi wa goli mbili kwa bila.
Magoli ya Man United katika mchezo huo yalifungwa Will Keane katika dakika ya 49 baada ya kipindi cha kwanza kushindwa kufungana na goli la pili likifungwa na Andreas Pereira katika dakika ya 58.
Mchezo huo pia uliwajumuisha wachezaji wapya wa Man United, kiungo Henrikh Mkhitaryan na beki Eric Bailly huku beki Luke Shaw ambaye aliumia mwanzoni kwa msimu wa 2015/2016 akirudi dimbani.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment